Tuesday, November 8, 2011

Mtoto anaesemekana kua ni wa Justin Beiber

 
Uvumi unaoendelea kupamba moto kwa sasa ni kua kuna mwanamke mwenye miaka 20 anadai mtoto wake mwenye miezi mi nne ni wa dogo Justin Beiber ambapo kwasasa team ya mwanamuziki huyo imeamua kutokukaa kimya na kuchukua hatua ya kwenda kuthibitisha Hospitalini na kama ni uwongo basi mwanadada huyo atachukuliwa hatua za kisheria kwasababu ijumaa iliopita Bwana mdogo Beiber alikataa uvumii huo kwa kusema kua kila anapofanyaga show akitoka anaenda direct kwenye gari na sio kuanza kutafuta wanawake wa kuondoka nao pia alisema anashangaa sana jinsi gani huyo mwanamke amekua mjasiri wa kuongea uongo mkubwa kama huo.........

Ila mwanamke huyo anatambulika kama Mariah Yeater aliendelea kukandamiza kwa kusema kua "Huyu mtoto ni wa Justin Beiber angalieni midomo yao inavyofanana! naomba mungu Justin azione picha hizi"

ila taarifa zilizopo chini ya kapeti ni kua mwanamke huyu sio mara ya kwanza kufanya tukio kama hili la kusingizia watu maarufu mtoto wake kwani ameshafanya hivyo kwa watu wawili ukiacha Justi Beiber...........




No comments:

Post a Comment